Waziri wa Michezo ashuhudia Mechi ya Maonesho ya wachezaji maarufu wa Soka wa Kimataifa na Misri


Dkt. Ashraf Sobhy, Waziri wa Vijana na Michezo, alishuhudia mechi ya maonesho iliyowakutanisha wachezaji maarufu wa Soka wa kimataifa chini ya uongozi wa mchezaji maarufu wa Italia Francesco Totti, na mchezaji maarufu wa Soka wa Misri chini ya uongozi wa kocha Hassan Shehata, huku ikilenga kufanya Misri kama kivutio cha michezo na utalii kimataifa.
Katika mechi hiyo, walishiriki wachezaji maarufu wa Soka, inajumuisha: Francesco Totti wa Italia, Julio Cesar wa Brazil, Marco Materazzi wa Italia, David Trezeguet wa Ufaransa, Gianluca Zambrotta wa Italia, Cafu wa Brazil, Alex wa Brazil, pamoja na wachezaji maarufu wa Soka wa Misri, kama vile kocha Hassan Shehata, kocha Ahmed Fathi, kocha Mohamed Barakat, kocha Essam El-Hadary, kocha Mohamed Nagui Gedo, kochai Abdel Sattar Sabry, kocha Hosny Abd Rabo, koccha Gamal Hamza, na kocha Hany Said, huku wakihudhuriwa na wanahabari na waandishi wa habari.
Kwa upande wake, Dkt. Ashraf Sobhy, alisema kuwa tukio hilo linaonyesha uongozi wa Misri katika ramani ya michezo ya kimataifa, na linakuza imani ya watu wa michezo wa kimataifa katika uwezo wetu wa kuandaa na miundombinu ya hali ya juu. Pia alisema kuwa kuwaleta wachezaji maarufu wa soka wa kimataifa kunachangia kukuza utalii wa michezo na kuleta mageuzi mazuri ya michezo kwa ujumla.
Waziri huyo pia alisema kuwa kuandaa shughuli kama hizi si tu kwa ajili ya kufanya Misri kama kivutio cha michezo na utalii, bali pia ina ujumbe wazi kuwa serikali ya Misri inaungaza mkono wanariadha wake, na inatoa mazingira bora ya kugundua vipaji na kukuza ujuzi wao kupitia kufanya kazi na wataalamu wa kimataifa. Wizara ya Vijana na Michezo inafanya kazi kwa bidii kuendeleza miundombinu ya michezo, si tu kwa ajili ya kurakibisha mashindano makubwa, bali pia kutoa fursa kwa vizazi vijijini kuthibitisha uwezo wao katika ngazi ya kimataifa.
Dkt. Ashraf Sobhy alisisitiza kuwa viongozi wa kisiasa wanatoa umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya michezo nchini Misri, kwa kuzingatia kuwa ni njia ya kuimarisha nguvu laini ya Misri, akionyesha kuwa kuwakaribisha wachezaji maarufu wa kimataifa katika michezo mbalimbali kunaimarisha nafasi ya Misri kama nchi inayoweza kuandaa na kukaribisha shughuli kubwa za michezo, na kuimarisha imani ya jumuiya ya kimataifa ya michezo katika uwezo wake wa kukaribisha mashindano ya kimataifa.
Pia, Waziri huyo aliwalika vijana wote kuchukua mfano wa mafanikio ya wachezaji maarufu hawa, akisisitiza kuwa serikali ya Misri itaendelea kuungaza mkono vipaji vya michezo katika michezo mbalimbali, na itawapa kila fursa iwezekanavyo kuwa mabalozi wa Misri katika mashindano za kimataifa za michezo.