Waziri wa Vijana na Michezo akutana na Rais wa Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari

Mhandisi Khaled Abdel Aziz, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari, alimpokea Dkt. Ashraf Sobhy, Waziri wa Vijana na Michezo, katika makao makuu ya Baraza huko Maspero.
Katika mkutano huo, njia za ushirikiano wa pamoja kati ya Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari na Wizara ya Vijana na Michezo zilijadiliwa katika hatua inayofuata, haswa katika uwanja wa michezo, ikizingatiwa jukumu lake kubwa katika kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu.
Waziri wa Vijana na Michezo Dkt. Ashraf Sobhy alimpongeza Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari, akimtakia mafanikio katika majukumu yake mnamo kipindi kijacho.
Akielezea umuhimu wa ushirikiano na mawasiliano na Baraza kufanya kazi ya kueneza maadili ya kimichezo na kukataa kuvumiliana na vurugu, huku akipongeza jukumu kubwa la Baraza katika kudhibiti vyombo vya habari vya michezo, hasa kwa kuzingatia maamuzi iliyoyatoa mnamo kipindi kilichopita.
Mhandisi Khaled Abdel Aziz alianza mkutano huo kwa kumkaribisha Dkt.Ashraf Sobhy, huku akionyesha nafasi kubwa iliyofanywa na Wizara ya Vijana na Michezo katika kutoa programu na shughuli mbalimbali za kusaidia vijana wa Misri, na kuongeza kuwa kiasi cha jukumu alichopewa Dkt. Ashraf Sobhy ni kubwa, hasa kwa vile sekta ya michezo ni muhimu na inafuatiliwa kila siku na wananchi.