Waziri wa Vijana na Michezo ahudhuria hafla ya kuwatayarisha maharusi 150 kutoka mkoa wa Giza

Waziri wa Vijana na Michezo Dkt.Ashraf Sobhy alihudhuria sherehe kubwa iliyoandaliwa na Chama cha watu cha kidemkrasia huko Giza iliyofanyika kwa kauli mbiu ya "Pamoja na Wananchi" kuandaa maharusi "150" kutoka kwa wasichana wa mkoa huo. ilifanyika jioni ya Jumanne, katika makao makuu ya Elimu ya utamaduni mnamo jiji la Oktoba 6, kwa mahudhurio ya Adel Al-Najjar, Gavana wa Giza Na kundi la viongozi wa Chama cha watu cha kidemkrasia huko Giza .
Dkt. Ashraf Sobhy alieleza furaha na hamu yake ya kushiriki katika sherehe hiyo, kwani hapo awali tulishiriki pia katika sherehe hiyo katika mkoa wa Gharbia.
Waziri huyo wa Vijana alieleza kuwa maadhimisho yanaakisi moyo wa mshikamano wa jamii, huku akipongeza juhudi za Chama cha watu cha kidemkrasia kwa kushirikiana na familia za Misri na kusaidia makundi yenye uhitaji zaidi kupitia mipango mahususi na ya kijamii inayofanya kazi ya kuwaunganisha watu wa Misri na kufikia maono ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri kuelekea kufikia utulivu wa kijamii kwa familia ya Misri.
Waziri huyo ameongeza kuwa maadhimisho yanasisitiza nafasi kubwa na madhubuti ya vyama vya kitaifa katika kuunga mkono jamii ya Misri huku akishukuru chama na uongozi wake kwa mchango wao wa kijamii kwa wana na mabinti wa familia ya Misri.