"Biashara kwa Vijana" Inafungua Milango Mpya kwa Masoko ya Bidhaa za Vijana na Ujasiriamali


Dkt. Ashraf Sobhy, Waziri wa Vijana na Michezo, ameshuhudia Matukio ya mkutano wa waandishi wa habari kutangaza uzinduzi wa toleo la pili la maonesho ya "Biashara kwa Vijana", yanayofanyika pamoja na udhamini wa Waziri Mkuu mnamo kipindi cha Januari 29 hadi Februari 8 ijayo, katika Uwanja wa Kimataifa wa Kairo, kwa ushiriki wa kundi la wajasiriamali vijana na wataalam katika ujasriamali na maendeleo ya uchumi.
Dkt. Ashraf Sobhy amesisitiza kuwa Wizara ya Vijana na Michezo kwa kushirikiana na taasisi za serikali ya Misri, inafanya kazi kuunga mkono ufundi wa mikono na kitamaduni ili kuchangia katika kuhifadhi utambulisho wa kitamaduni wa Misri, pamoja na kutoa msaada kwa miradi mipya na kuwawezesha vijana kukuza mawazo yao na kuyabadilisha kuwa miradi ya kiuchumi yenye mafanikio.
Na aliashiria kuwa Wizara inalipa kipaumbele kikubwa kwa kuimarisha jukumu la viwanda vya kitaifa kupitia ubunifu na maendeleo, ili kufikia ongezeko la thamani kwa bidhaa za kitaifa na kuchangia katika kuimarisha nafasi yake katika masoko ya ndani na ya kimataifa.
Akiongeza kuwa Wizara ya Vijana na Michezo inafanya kazi kupitia mipango hii yenye ahadi kutoa fursa mpya za ajira kwa vijana, katika mfumo wa mpango wa serikali wa kupunguza viwango vya ukosefu wa ajira, na kuhamasisha vijana kutumia uwezo wao na nguvu zao katika kuunda mustakabali bora kwa wao wenyewe na kwa taifa.
Na Waziri wa Vijana na Michezo alihitimisha hotuba yake akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta zote kuunga mkono vijana kufikia malengo yao ya kiuchumi na kiufundi, na kuchangia katika kujenga uchumi wa kitaifa wenye nguvu unaotegemea ubunifu na ujasriamali.