Waziri wa Michezo akutana na Viongozi wa Kikundi cha Hoteli za Plaza Inn


Waziri wa Vijana na Michezo, Dkt. Ashraf Sobhy alikutana na wawekezaji wengi wa sekta binafsi " Kampuni ya Plaza Inn inayohusika na kuendeleza miundombinu ya vijana katika Wizara ya Vijana na Michezo ili kusimamia na kutoa huduma za hoteli kwa kiwango cha juu, na kuendana na huduma zinazotolewa na hoteli sawa na hoteli zenye huduma za nyota tano Kwa vijana na familia ya Misri ndani ya miji ya vijana katika mikoa mbalimbali ya Jamhuri na kwa ushirikiano na Idara kuu ya Miji ya Vijana inayoongozwa na Meja Jenerali Abdel Rahman Shalash.
Maafisa wa Hoteli ya Plaza walionesha mapendekezo ya kazi za maendeleo kutekelezwa katika Kituo cha Maendeleo ya Vijana huko Al-Jazirah, katika Zamalek, na Hoteli ya Elimu ya Kiraia, itakayosaidia katika kuendeleza huduma na kuandaa vyumba vya hoteli kwa kiwango cha juu.
Sobhy alisisitiza kuendelea kufanya kazi katika kuendeleza miradi ya vijana na michezo katika mikoa yote ya jamhuri, kwa njia ambayo inakidhi matarajio ya vijana na familia za Misri.
Mkutano huo pia ulijadili maendeleo ya hosteli za vijana katika mkoa wa Matrouh.
Waziri wa Vijana na Michezo alieleza kuwa tunataka kutoa huduma jumuishi kwa vijana na watoto, na kwamba huduma zitakazotolewa zitawanufaisha vijana wa mkoa na mikoa ya jirani, jambo ambalo litasaidia shughuli mbalimbali za vijana, michezo na utamaduni na linafanya mkoa wa Matrouh kuvutia kwa shughuli za vijana na michezo wakati wote wa mwaka.
Waziri huyo alieleza kuwa Wizara inalenga kuendeleza na kuanzisha Hosteli ya Matrouh ili iwe moja ya vinara wa vijana nchini Misri na mkoa wa Matrouh, ili iwe kivutio kwa wageni wote wa hosteli za vijana nchini Misri.
Msaidizi wa Waziri wa Sekta ya Vijana, Meja Jenerali Ismail Al-Far, Mkuu wa Utawala Mkuu wa Miji ya Vijana, Meja Jenerali Abdul Rahman Shalash,Waziri Msaidizi wa Uwekezaji, Dkt. Zakaria Mohie,Msaidizi wa Waziri wa Masoko na Uwekezaji, na Dkt. Abdullah Al-Bahar walihudhuria Mkutano huo.